ULIMWENGU
1 dk kusoma
Israel yaitaka Marekani kujiunga na 'kampeni ya kijeshi' dhidi ya Iran: ripoti
Kwa mujibu wa afisa mmoja wa Marekani, utawala wa Trump kwa sasa haufikirii kujiunga na operesheni za kijeshi.
Israel yaitaka Marekani kujiunga na 'kampeni ya kijeshi' dhidi ya Iran: ripoti
Afisa wa Marekani, kwa mujibu wa Axios, alithibitisha kwamba Israel iliomba Washington kujiunga na operesheni ya kijeshi. Picha: AP / AFP
15 Juni 2025

Israel imeitaka Marekani kujiunga na kampeni yake mpya ya kijeshi dhidi ya Iran, iliripoti Axios.

Likinukuu vyanzo vya Marekani na Israel, chombo hicho cha habari kilisema Israel haina uwezo wa kuharibu eneo la kurutubisha madini ya uranium la Iran la Fordow, ambalo limezikwa ndani kabisa ya mlima, na linahitaji usaidizi wa Marekani kulilenga vyema siku ya Jumapili.

Afisa wa Marekani, kwa mujibu wa Axios, alithibitisha kwamba Israel iliiomba Washington ijiunge na operesheni hiyo ya kijeshi lakini akasema utawala kwa sasa hautilii maanani.

Kikinukuu chanzo cha Israel, chombo hicho cha habari kiliripoti hapo awali kwamba Rais wa Marekani Donald Trump alipendekeza uwezekano wa Marekani kushiriki ikiwa ni lazima wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.

Hata hivyo, afisa wa Ikulu ya White House alikanusha madai hayo siku ya Ijumaa. Washington imekuwa ikisema mara kwa mara kwamba Israel ilichukua hatua peke yake katika hatua zake za hivi karibuni za kijeshi dhidi ya Iran.


CHANZO:TRT Afrika and agencies
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us