21 Julai 2025
Maluki alimshinda katibu mkuu anayeondoka Francis Mutuku katika uchaguzi uliofanyika siku ya Jumatatu.
Maluki, ambaye alikuwa makamu wa kwanza wa Kamati ya Olimpiki, alipata kura 15 kutoka kwa mashirikisho 27 yaliyowakilishwa, huku Mutuku, akifanikiwa kupata kura 12.
Shadrack anachukua nafasi ya Paul Tergat, mwanariadha mstaafu wa mbio za masafa marefu ambaye amemaliza muda wake.
Maluki pamoja na maafisa wengine wa nyadhifa mbalimbali kwenye kamati yake wanatarajiwa kusimamia maandalizi ya Olimpiki ijayo, hasa wakizingatia kuimarisha wanamichezo, uwazi, na matokeo ya Kenya katika michezo hiyo ulimwenguni.