Mambo matano yakuhusu mlima Kilimanjaro:
1. Ni mlima ndefu zaidi duniani inayosimama pasina milima mengine karibu
Ukiwa na urefu wa mita 5,895, Mlima Kilimanjaro sio tu mlima mrefu zaidi barani Afrika lakini pia mlima mrefu zaidi uliojisimamia ulimwenguni. Tofauti na milima mengine zilizo katika safu ya milima, Kilimanjaro inasimama peke yake, na kufanya asili yake kuwa wa kushangaza zaidi.
2. Ina na Koni Tatu za Volcano, moja ikiwa na uwezo wa kulipuka
Kilimanjaro inajumuisha koni tatu tofauti za volkeno: Kibo, Mawenzi, na Shira. Kibo, kilicho juu zaidi, kinaweza kulipuka tena, huku Mawenzi na Shira zikiwa zimepoteza uwezo wa kulipuka. Utatu huu wa koni za volkeno huchangia katika topografia ya kipekee ya mlima na umuhimu wa kijiolojia.
3. Maeneo Mbalimbali ya Kiikolojia
Kupanda Kilimanjaro ni sawa na kusafiri kutoka ikweta hadi Arctic. Ukiiapanda utapitia katika maeneo matano tofauti ya ikolojia: ardhi iliyolimwa, msitu wa mvua, joto, jangwa la alpine, na kilele cha aktiki. Mabadiliko haya kwa anayepanda huonesha mifumo mbalimbali ya ikolojia katika safari moja.
4. Barafu yake inapungua kwa kasi
Licha ya kuwa karibu na ikweta, kilele cha Kilimanjaro kina barafu. Lakini, barafu ya Mlima Kilimanjaro inapotea haraka. wanasayanasi wanakisia kuwa kufika 2060, barafu yote ya mlima kilimanjaro itakuwa umeyeyuka.
5. Inawakilisha Afrika katika Milima saba kuu ya dunia yaani ‘Seven Summits’.
Orodha hii hufuatiliwa na wanaopenda kupanda milima. Mlima kilimanjaro hupokea watu kati ya 35,000 to 50,000 kwa mwaka wanaokwea na kufika viwango tofauti. Kupanda hadi kilele huchukua takriban siku 9.