AFRIKA
1 dk kusoma
Kenya Airways ya Nairobi- Dar es Salaam ililazimika kurudi JKIA kutokana na dharura ya kiafya
Ndege hiyo ya KQ484 ilirudishwa uwanja wa Jomo Kenyatta lakini baada ya itifaki za kiafya kutimizwa iliruhusiwa kuendelea na safari yake saa mbili baadaye.
Kenya Airways ya Nairobi- Dar es Salaam ililazimika kurudi JKIA kutokana na dharura ya kiafya
Ndege ya Kenya Airways ililazimika kurudi uwanja wa JKIA kutokana na tishio la kiafya / Reuters
27 Aprili 2025

Ndege ya Kenya Airways iliyokuwa ikielekea Dar es Salaam kutoka Nairobi ililazimika kurudi kutua uwanja wa Jomo Kenyatta baada ya tukio la kiafya, kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na shirika hilo kwenye mtandao wa X.

Taarifa hiyo ilisema kuwa maafisa wa afya na walipokea ndege hiyo huku wakiimarisha itifaki za kiafya kudhibiti tukio hilo.

Baada ya saa mbili ya kusibiri ndege hiyo iliruhusiwa kuendelea na safari yake kwenda Dar es Salaam.

‘‘Usalama na ustawi wa wageni na wafanyakazi wetu unasalia kuwa kipaumbele chetu cha juu zaidi’’ ilisema taarifa hiyo.

Japo kumekuwa na uvumi katika baadhi iya vyombo vya habari, Kenya Airways haikutaja sababu ya dharura hiyo.

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us