Sekeseke la kisheria ambalo wataalamu wa sheria kuhusu masuala ya Israel wamekuwa wakionya sasa linaelekea kutimia. Siku hiyo hiyo mataifa 27 ya Magharibi yametoa taarifa kwa umma yakionya kuhusu “hatua zaidi” yakiunga mkono kusitishwa kwa mapigano ya Gaza, wanajeshi wawili wa Israel wanaoshtumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita walikamatwa na kuhojiwa na mamlaka za Ubelgiji.
Katika sheria ya kimataifa, mataifa yanaweza kuwajibishwa kwa uhalifu kwa njia moja au mbili: nchi yenyewe inaweza kuwekewa vikwazo na mashirika ya kimataifa, na maafisa wake na watendaji wake ambao wametekeleza, kuamrisha, kusaidia, kuruhusu, au kusaidia katika uhalifu kama huo wanaweza kushtakiwa katika mahakama za kimataifa au za nyumbani.
Wiki iliopita, Mkutano wa dharura wa kundi la The Hague uliwaleta pamoja mataifa mjini Bogota, Colombia, na kutaka hatua zaidi zichukuliwe badala ya kushtumu tu na kutaka kuchukuliwe hatua za pamoja kwa kuzingatia sheria ya kimataifa.
Kamata kamata ya Ubelgiji ilisaidiwa na Wakfu wa Hind Rajab na shirika la Global Legal Action Network (GLAN), ambayo yanafanya kazi kama hiyo katika maeneo mbalimbali. Mashirika yote yamehusika na uchunguzi katika siku za nyuma ambao ulilazimisha mwanajeshi wa Israel ambaye alikuwa mapumzikoni Brazil kukimbia mwaka uliopita, na wanajeshi wawili kukimbia mjini Amsterdam mwezi Februari.
Ujumbe uko wazi: Wanajeshi wa Israel wanaoshtumiwa kwa uhalifu Gaza hawana uhakika lini watafikiwa.
Hatua hii ndiyo mwanzo wa kukomesha uhalifu huu — na kuanzishwa kwa hatua za kisheria na kisiasa za kuwawajibisha Israel kwa uhalifu wao huko Gaza, ambapo wanajeshi wake wamewaua watu zaidi ya 59,000 – wengi wao wakiwa wanawake na watoto – kwa zaidi ya miezi 21?
Israel kizimbani
Kuna sababu ya kufikiria kuwa watunga sera katika mataifa ya Magharibi kama yanaweza kubadilisha sera zake kwa Israel.
Waziri Mkuu wa Uingereza Sir Keir Starmer amekuwa katika shinikizo la kutambua Taifa la Palestina kutoka kwa baraza lake la mawazir, kabla ya "kila kuangamizwa na kutokuwa na cha kutambuliwa”.
Swali kuu ni kama mataifa yataenda zaidi ya kutambua kwa maneno na kuchukuwa hatua madhubuti za kuwawajibisha Israel.
Licha ya Marekani kumuwekea vikwazo mwendesha mashtaka wa mahakama ya ICC na majaji, wanaochunguza madai ya Israel ya uhalifu wa kivita uhalifu dhidi ya binadamu Gaza na maeneo mengine.
Kabla hajaondoka kwa muda, mwendesha mashtaka alitangaza kuwa ofisi yake inaangazia uhalifu siyo tu Gaza, bali pia katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa.
Viongozi wa Israel wa mrengo wa kulia, ikiwemo Bezalel Smotrich na Itamar Ben-Gvir, wametoa kauli za wazi wakieleza msimamo wao wa kuhalalisha uhalifu dhidi ya binadamu, na wamewekewa vikwazo na EU na serikali za Australia, Canada, New Zealand, Norway na Uingereza.
Kulingana na taarifa katika jarida la The Wall Street Journal, mwendesha mashtaka wa ICC amekuwa akiandaa hati za kuwakamata viongozi waandamizi wanaoongoza ukaliaji Palestina kabla ya kwenda likizo.
Huku wasambazaji wakuu wawili wa silaha kwa Israel – Marekani na Ujerumani – wakiwa hawako miongoni mwa mataifa 27 ya Magharibi yalitoa onyo la hivi karibuni, wote wako kwenye shinikizo kubadilisha msimamo wao.
Taarifa hiyo iliyotolewa mwezi Juni na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa Francesca Albanese (ambaye amewekewa vikwazo na utawala wa Trump) kwa wanachofanya kwa mashirika (ambayo mengi ni ya Wamarekani) katika kuendelea kuunga mkono uhalifu katika maeoneo yaliyokaliwa ya Palestina na ameonya mashirika hayo – kuwa wanaweza kuwa washirika wa mauaji ya halaiki ya Israel kama hawatosita kuunga mkono biashara za Israel.
Tayari, KLP, kampuni kubwa ya Norway ya pensheni, ina historia ya siku nyingi ya kutumika kusaidia Jeshi la Israel kuharibu nyumba za Wapalestina.
Nchini Uholanzi, malalamiko ya uhalifu yaliyowasilishwa kwa Mwendesha Mashtaka wa nchini na mashirika kadhaa yasiyokuwa ya kiserikali yameshtumu booking.com, kampuni ya tiketi ya mtandaoni, kwa kuhusika na kutakatisha fedha na kufaidika na uhalifu wa kivita kwa kusaidia kukodishwa kwa nyumba za Waisrael katika ardhi inayokaliwa na kuibiwa kutoka kwa Wapalestina.
Mambo yanabadilika?
Ujerumani, nchi ya pili kwa ukubwa katika kuwapa silaha Israel, sasa hivi inajitetea katika kesi iliyowasilishwa dhidi yao na Nicaragua katika Mahakama ya Kitaifa ya Haki (ICJ), mahakama nyingine ya kudumu ya kimataifa mjini The Hague.
Wakati huohuo, Israel inakabiliwa na uhalifu mbaya zaidi kuwahi kutokea kwa binadamu kutoka kwa Afrika Kusini kwenye kesi iliyowasilishwa ICJ.
Kwa sasa, hatua za kuwawajibisha Israel zinatarajiwa kuendelezwa katika mahakama za kimataifa na mataifa yenye uchumi mdogo, licha ya kuwa kamata kamata ya Ubelgiji na malalamiko ya uhalifu dhidi ya makampuni Uholanzi yanaweza kuashiria kuwa mataifa mengine yana wasiwasi kuhusu uhalifu unaokithiri wa Israel na kuimarisha msimamo wao – hasa wakati njaa kali inapoikabili Gaza.
Uungwaji mkono duniani ambao Israel ulipata mwaka mmoja uliopita – kabla ya kuwaua viongozi waandamizi wa Hamas, kuwakabili Hezbollah Lebanon, kushambulia vinu vya nyuklia Iran, na kambi za kijeshi za Syria na Yemen – unaonekana kudhoofika.
Ijapokuwa wamechelewa, baadhi ya watunga sera wa Magharibi na wanasheria waandamizi wamekuja kugundua kuwa vita vya Gaza havikuwa kuhusu haki ya Israel “kujitetea” lakini kuwaadhibu Wapalestina kwa ujasiri wao na uthubutu wa kukaa ngangari katika ardhi ya mababu zao.