Mji wa Uturuki wa Gaziantep umeshinda Tuzo ya Ulaya 2025
Mji wa Uturuki wa Gaziantep umeshinda Tuzo ya Ulaya 2025
Tuzo ya Ulaya imeasisiwa mwaka 1955 na Baraza la Bunge la Ulaya, ni Tuzo ya juu kabisa kwa miji ya Ulaya.
9 Aprili 2025

Tuzo ya mwaka 2025 ya Ulaya imetolewa kwa mji wa Kituruki wa Gaziantep, uliopo kusini mashariki, Baraza la Bunge la Ulaya limetangaza (PACE).

Tuzo hiyo inatolewa kila mwaka kwa mji ambao uko mstari wa mbele katika kukuza misingi ya Ulaya.

Katika taarifa ya Jumanne, PACE imesema Gaziantep ambayo ina miji washirika 25, ikiwemo Duisburg ya Ujerumani, Celje ya Slovenia, Ostrava ya Jamhuri ya Czech na Braga ya Ureno.

“Ni kitovu cha uchumi, unaojulikana kwa sekta ya viwanda, na uzalishaji wa nguo, na ni mji wa kwanza Uturuki kutekeleza mpango kazi dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi,” imesema taarifa.

PACE imesema, Gaziantep pia imejitika katika ukuaji wa mji, uhifadhi wa mazingira na maisha bora kwa wakazi wake.

Hii ikizingatiwa kwamba, mji huo awali uliwekwa katika kiwango bora cha Ulaya katika Utawala Bora, taarifa hiyo imesema ni mjumbe wa 28 wa mtandao wa kimataifa ikiwemo Eurocities, Energy Cities, UNESCO, na muungano wa Manispaa za Uturuki.

Tuzo hiyo inajumuisha medali, na fedha zitakazotumika kutembelea taasisi za ulaya kwa vijana kutoka miji iliyoshinda.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us