AFRIKA
1 dk kusoma
Uganda kuleta sheria itakayoruhusu raia kushtakiwa mahakama ya kijeshi
Kizza Besigye anashikiliwa na serikali ya Uganda kwa tuhuma za uhaini na umiliki wa silaha bila kibali.
Uganda kuleta sheria itakayoruhusu raia kushtakiwa mahakama ya kijeshi
Kiongozi wa upinzani Uganda Kizza Besigye / REUTERS
18 Aprili 2025

Serikali ya Uganda inakusudia kupitisha sheria itakayoruhusu mahakama za kijeshi kusikiliza kesi za raia kwa kesi maalumu licha ya Mahakama ya Juu nchini humo kupinga hatua hiyo Januari 31, 2025.

"Sheria hiyo, ambayo itafafanua “hali ya kipekee ambayo raia anaweza kuhukumiwa kwa sheria ya kijeshi,” imeandaliwa na inasubiri idhini ya baraza la mawaziri kabla ya kuwasilishwa bungeni," Nobert Mao, Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba aliliambia Bunge.

Serikali inashinikiza kuifufua kupitia Mswada wa UPDF (Marekebisho) wa 2025.

Iwapo itapitishwa, sheria hiyo mpya itaruhusu serikali kumrudisha mpinzani Kizza Besigye kwenye mahakama ya kijeshi.

Kizza Besigye anashikiliwa na serikali ya Uganda kwa tuhuma za uhaini na umiliki wa silaha bila kibali.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us