MAISHA
1 dk kusoma
Janga la unene
Katika muda wa miaka 25 tu, mtu mzima mmoja kati ya watu wawili anaweza kuwa na unene wa kupitiliza.
Janga la unene / TRT Afrika Swahili
10 Julai 2025

Hiyo ina maana kwamba mimi au wewe tunaweza kuwa miongoni mwao.  

Utafiti mpya unaonyesha kwamba iwapo hakutakuwa na mabadiliko makubwa katika mfumo wa maisha, basi takriban asilimia 60 ya watu duniani kufikia mwaka 2050 watakuwa na unene wa kupitiliza. 

Takwimu zinatabiri kwamba theluthi moja ya vijana wanene wanaweza kutoka Afrika Kaskazini, Mashariki ya Kati, Amerika Kusini na nchi za Karibiani. 

Lakini sio hilo tu, utafiti unataka hatua zaidi zichukuliwe ili kubadilisha mifumo ya afya kote ulimwenguni. 


Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us