23 Juni 2025
Timu nyingine iliyofuzu katika hatua hiyo kutoka kundi G ni Juventus. Juventus iliwafunga Wydad Casablanca ya Morocco magoli 4-1 Jumapili.
City na Juventus watakutana kwenye mechi yao ya makundi jijini Orlando siku ya Alhamisi kubaini nani ataibuka mshindi wa kundi hilo.
Atakayemaliza wa kwanza kundi G atacheza dhidi ya atakayemaliza wa pili kwenye kundi H. Atakayekuwa wa kwanza kwenye kundi H atakabiliana na aliyemaliza nafasi ya pili kwenye kundi G.
Tayari Real Madrid ya Hispania imefuzu kwa hatua hiyo ya mtoano, sawa na Red Bull Salzburg ya Austria kutoka kwenye kundi H. Timu zingine kwenye kundi hilo ni Al-Hilal ya Saudia Arabia na Pachuca kutoka Mexico.