AFRIKA
2 dk kusoma
Uganda yawahamisha raia wake 42 kutoka Iran
Serikali ya Uganda inasema kuwa Kituo cha Kuratibu Uokoaji wa Dharura kilianzishwa kwa haraka nchini Uturuki ili kuwezesha usajili, uratibu na harakati salama za raia wa Uganda.
Uganda yawahamisha raia wake 42 kutoka Iran
Uganda imewaondoa raia wake kutoka Iran / picha: Serikali ya Uganda / Public domain
20 Juni 2025

Serikali ya Uganda kupitia Ubalozi wake mjini Tehran, imesema imefanikiwa kuratibu zoezi la kuwaondoa salama raia 42 wa Uganda na wafanyakazi wawili wa kidiplomasia kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hadi Jamhuri ya Uturuki.

Hii inafuatia kuzuka kwa mapigano kati ya Iran na Israel tarehe 13 Juni 2025, ambayo yameathiri pakubwa hali ya usalama katika eneo hilo.

“Mchakato wa kuwahamisha watu hao uliongozwa na Ubalozi wa Uganda mjini Tehran, chini ya uongozi wa Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Nje mjini Kampala, na kwa usaidizi mkubwa kutoka Ubalozi wa Uganda mjini Ankara, Uturuki.”

Serikali ya Uganda inasema kuwa Kituo cha Kuratibu Uokoaji wa Dharura kilianzishwa kwa haraka nchini Uturuki ili kuwezesha usajili, uratibu na harakati salama za raia wa Uganda.

“Katika onyesho la mfano la ushirikiano na mwitikio, Jamhuri ya Uturuki ilikubali ombi la Uganda la kutoa visa wakati wa kuwasili watu walioathirika, kuruhusu usafiri wao wa haraka na kuingia kwa muda katika eneo la Uturuki kama sehemu ya mchakato wa kuwahamisha,” Serikali ya Uganda imesema.

Usafiri wa ardhini kutoka Tehran hadi Uturuki ulipangwa, na kundi la kwanza lilipokelewa kwa mafanikio kwenye mpaka wa Bargarzan Jumatano, 18 Juni 2025.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda imesema wanafunzi 42 wa Uganda na wafanyakazi wawili wa Ubalozi kwa sasa wako katika usafiri wa kuelekea Istanbul, ambako wameratibiwa kupanda ndege ya kukodi kurudi nyumbani Uganda.

CHANZO:TRT Swahili
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us