ULIMWENGU
2 dk kusoma
Trump anasema Israel na Iran zilikubali kusitisha mapigano, lakini mapigano yanaendelea
Milipuko imesikika Beersheba, Tel Aviv na Israel ya kati.
Trump anasema Israel na Iran zilikubali kusitisha mapigano, lakini mapigano yanaendelea
Trump alitangaza kusitishwa mapigano japo pande zote mbili zimeendelea kushambuliana / Picha: Reuters
24 Juni 2025

Iran yarusha wimbi la tano la makombora, 3 yauawa kusini mwa Israel Jeshi la Israel linasema kuwa wimbi la tano la makombora limerushwa kutoka Iran kuelekea Israel.

Huduma ya dharura ya Israel Magen David Adom (MDA), imesema takriban watu watatu wameuawa katika shambulio la kombora katika mji wa Beersheba kusini mwa Israel (Be'er Sheva) - ikiwa ni vifo vya kwanza kuripotiwa tangu Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kusitisha mapigano kati ya nchi hizo mbili siku ya Jumatatu.

"Kufuatia eneo la maafa ya makombora kusini mwa Israel: Kufikia sasa, timu za MDA zimetangaza vifo vya watu watatu - watu wawili walio na majeraha ya wastani wamehamishwa hospitalini, na takriban watu sita wenye majeraha madogo wanatibiwa katika eneo la tukio," Magen David Adom alisema katika taarifa yake kwenye X.

Milipuko pia ilisikika Tel Aviv na Israel ya kati.

Mashambulizi ya hivi punde yanakuja saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuwa Israel na Iran zimekubaliana kusitisha mapigano kwa awamu kwa lengo la kumaliza kile alichokiita "vita vya siku 12." Hata hivyo, hakuna thibitisho rasmi wa makubaliano hayo kutoka Tehran.

Wakati huo huo TV ya Iran ilitangaza kuwa Israel imemuua mwanasayansi wa nyuklia Mohammad Reza Siddiqi katika mashambulizi yake ya hivi majuzi.

CHANZO:TRT World
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us