9 Juni 2025
Mlipuko wa ugonjwa wa mpox bado ni tatizo la dharura la kiafya, Shirika la Afya Duniani lilisema Jumatatu, huku Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo akitoa utaratibu mpya pamoja na mapendekezo ya muda ya kufuatwa.
Mara ya kwanza kwa WHO kutangaza ugonjwa huo kuwa dharura ilikuwa mwezi Agosti mwaka uliopita, wakati mlipuko wa aina tofauti ya mpox ulipoibuka na kuenea kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hadi katika mataifa jirani.
Kutangaza hali ya dharura kwa afya ya umma kimataifa ni onyo la hali ya juu la tahadhari kutolewa na WHO.