UTURUKI
1 dk kusoma
Ushirikiano wa kina umeongeza biashara kati ya Uturuki na EU: Waziri
Biashara za pamoja zimefikia dola bilioni 220 huku Uturuki na EU zikiandaa kuzindua mazungumzo ya kiwango cha juu mjini Ankara, yenye lengo la kusasisha Ushuru wa Pamoja na kuondoa vikwazo vya biashara.
Ushirikiano wa kina umeongeza biashara kati ya Uturuki na EU: Waziri
Uturuki na Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuitisha mkutano wa pili wa Mazungumzo ya Juu ya Biashara Julai 1, 2025 Ankara. (Picha: AA) / AA
5 Juni 2025

Wizara ya Biashara ya Uturuki imetangaza kwamba “ajenda chanya” katika uhusiano wa kibiashara na Umoja wa Ulaya inaendelea kupanuka, huku kukiwa na ushirikiano zaidi unaoonekana katika ukuaji wa viwango vya biashara ya pamoja.

Tangazo hilo limetolewa Jumatano baada ya Waziri wa Biashara wa Uturuki Omer Bolat kukutana na Kamishna wa Biashara wa EU Maros Sefcovic pembezoni mwa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa OECD mjini Paris, ambapo wamejadiliana kuhusu mabadiliko ya biashara ya dunia na jinsi mafungamano ya kiuchumi kati ya Uturuki-EU yanavyoweza kwenda sambasamba na kuimarika.

Mazungumzo ya kina Ankara

Kwa mujibu wa Wizara, pande zote mbili zimekubaliana kuitisha mkutano wa pili wa Mazungumzo ya Biashara ya Ngazi ya Juu yatakayofanyika Julai 1, 2025, mjini Ankara, kwa ushiriki wa wafanyabiashara na asasi za kiraia.

Hii ina lengo la kusukuma mbele mapendekezo ya ushirikiano na kutatua changamoto muhimu za biashara, ikiwemo changamoto za viza wanazozipata wajasiriamali wa Uturuki katika eneo la Schengen la EU.

Ajenda hiyo pia imegusia vipaombele vya pamoja vya biashara, maendeleo katika Ushuru wa Pamoja, na jitihada za kubaliana na vikwazo vya pamoja vya biashara-katika maeneo ambayo kumekuwa na maendeleo makubwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us