Wizara ya Biashara ya Uturuki imetangaza kwamba “ajenda chanya” katika uhusiano wa kibiashara na Umoja wa Ulaya inaendelea kupanuka, huku kukiwa na ushirikiano zaidi unaoonekana katika ukuaji wa viwango vya biashara ya pamoja.
Tangazo hilo limetolewa Jumatano baada ya Waziri wa Biashara wa Uturuki Omer Bolat kukutana na Kamishna wa Biashara wa EU Maros Sefcovic pembezoni mwa mkutano wa Baraza la Mawaziri wa OECD mjini Paris, ambapo wamejadiliana kuhusu mabadiliko ya biashara ya dunia na jinsi mafungamano ya kiuchumi kati ya Uturuki-EU yanavyoweza kwenda sambasamba na kuimarika.
Mazungumzo ya kina Ankara
Kwa mujibu wa Wizara, pande zote mbili zimekubaliana kuitisha mkutano wa pili wa Mazungumzo ya Biashara ya Ngazi ya Juu yatakayofanyika Julai 1, 2025, mjini Ankara, kwa ushiriki wa wafanyabiashara na asasi za kiraia.
Hii ina lengo la kusukuma mbele mapendekezo ya ushirikiano na kutatua changamoto muhimu za biashara, ikiwemo changamoto za viza wanazozipata wajasiriamali wa Uturuki katika eneo la Schengen la EU.
Ajenda hiyo pia imegusia vipaombele vya pamoja vya biashara, maendeleo katika Ushuru wa Pamoja, na jitihada za kubaliana na vikwazo vya pamoja vya biashara-katika maeneo ambayo kumekuwa na maendeleo makubwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.