ULIMWENGU
1 dk kusoma
Uingereza yawawekea vikwazo maafisa wawili wa Israeli kwa matamshi yao kuhusu Gaza: Taarifa
Waziri wa usalama na waziri wa fedha 'walichochea vurugu za misimamo mikali na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu za Wapalestina,' alisema David Lammy
Uingereza yawawekea vikwazo maafisa wawili wa Israeli kwa matamshi yao kuhusu Gaza: Taarifa
Itamar Ben-Gvir ni waziri wa usalama wa Israeli. / Reuters
10 Juni 2025

Uingereza imewawekea vikwazo mawaziri wawili wa Israeli wa siasa za mrengo wa kulia kwa matamshi yao kuhusu Gaza, vyombo vya habari viliripoti siku ya Jumanne.

Waziri wa Usalama Itamar Ben-Gvir na Waziri wa Fedha Bezalel Smotrich watakabiliwa na marufuku ya kusafiri na mali zao zitapigwa tanchi kama sehemu ya hatua zilizotangazwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza David Lammy.

Wawili hao "walichochea vurugu za misimamo mikali na ukiukwaji wa haki za binadamu za Wapalestina," alisema Lammy, kama ilivyoripotiwa na shirika la habari la BBC.

Kwa mujibu wa taarifa, wakijibu kuhusu vikwazo hivyo, Israeli imesema "ni makosa sana kwa wawakilishi waliochaguliwa na watu na maafisa wa serikali kuchukuliwa hatua za aina hii."

CHANZO:AA
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us