AFRIKA
3 DK KUSOMA
Nigeria yasitisha ziara ya Waziri Mkuu wa Czech kwa sababu ya 'uwezo duni wa mapokezi'
Hata hivyo, vyombo vya habari vya Czech viliripoti kwamba kukataa kwa serikali ya Nigeria kumpokea Fiala na ujumbe wake, kunahusishwa na msimamo wa Prague wa kuiunga mkono Israel.
Nigeria yasitisha ziara ya Waziri Mkuu wa Czech kwa sababu ya 'uwezo duni wa mapokezi'
Waziri Mkuu wa Czech Petr Fiala alitarajiwa kuzuru Nigeria kwa siku mbili. / Picha: AFP / Picha: Reuters / Others
8 Novemba 2023

Nigeria imeghairi ziara ya Waziri Mkuu wa Czech Petr Fiala na ujumbe wake wa kibiashara dakika ya mwisho, kwa sababu ya kutokuwa na uwezo wa serikali kuwapa mapokezi ya kutosha.

Hata hivyo, vyombo vya habari vya Czech viliripoti Jumanne kwamba kukataa kwa serikali ya Nigeria siku ya Jumatatu, siku moja tu kabla ya ziara ya Fiala na ujumbe wake wa kibiashara, kunahusishwa na msimamo wa Prague wa kuiunga mkono Israel katika Umoja wa Mataifa kuhusu mzozo unaoendelea wa Israel na Palestina.

Serikali ya Nigeria imewafahamisha kuwa haiwezi kutoa mapokezi na programu ifaayo kwa Fiala na ujumbe wake wa kibiashara.

Kulingana na hili, waliamua kughairi ziara hiyo, msemaji wa serikali ya Czech Vaclav Smolka aliwaambia waandishi wa habari mjini Nairobi, mji mkuu wa Kenya, ambako walifika baada ya kuzuru Ethiopia, kulingana na chombo cha habari cha Irozhlas.

Ziara ya serikali ya siku mbili

Waziri mkuu na ujumbe wake walipangiwa kuwasili nchini Nigeria siku ya Jumanne kwa ziara rasmi ya siku mbili.

Hata hivyo, Irozhlas alinukuu vyanzo vya kidiplomasia katika ripoti yake, vikieleza kuwa hatua ya Nigeria inaweza kuwa inahusiana na sera za wazi za serikali ya Czech zinazoiunga mkono Israel, wakati Israel inakabiliwa na ukosoaji unaokua wa kimataifa.

Imeongeza kuwa Jamhuri ya Czech, pamoja na Marekani na Israel, ni miongoni mwa nchi 14 zilizopiga kura kupinga azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la kutaka kusitishwa mara moja kwa mapigano kwa maslahi ya kibinadamu huko Gaza mnamo Oktoba 27.

Israel ilianzisha mashambulizi ya anga na ardhini kwenye Ukanda wa Gaza kufuatia shambulio la kuvuka mpaka la Hamas tarehe 7 Oktoba.

Maelfu waliuawa, wengi wao wakiwa watoto

Takriban Wapalestina 10,328 wakiwemo watoto 4,237 na wanawake 2,719 wameuawa. Idadi ya vifo vya Israeli, wakati huo huo, ni karibu 1,600, kulingana na takwimu rasmi.

Kando na idadi kubwa ya majeruhi na watu wengi waliokimbia makazi yao, vifaa vya msingi vinapungua kwa wakazi milioni 2.3 wa Gaza kutokana na mzingiro wa Israel.

➤ Fuatilia TRT Afrika Swahili kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us