AFRIKA
2 DK KUSOMA
Henry Kissinger, mwanadiplomasia wa Marekani, na mshinid wa Nobel aliyezua utata, afariki akiwa na miaka 100
Kissinger, ambae amefariki Connecticut, alijulikana kwa uhodari wake na ubobefu mpana, lakini pia alionekana kama mhalifu wa kivita kutokana na uungaji mkono wake wa udikteta, hasa Latin America.
Henry Kissinger, mwanadiplomasia wa Marekani, na mshinid wa Nobel aliyezua utata, afariki akiwa na miaka 100
Wajumbe wawili wa kamati ya Tuzo ya Nobel walijiuzulu kufutia uteuzi na maswali yaliibuka kuhusu shambulizi la Marekani la siri Cambodia. / Picha: Reuters 
30 Novemba 2023

Henry Kissinger, mshindi wa Nobel aliyezua utata na mwanadiplomasia nguli ambae uhudumu wake chini ya maraia wawili umeacha alama katika sera za mambo ya nje za Marekani, amefariki akiwa na umri wa miaka 100, Kissinger Associates Inc imesema katika taarifa yake.

Amekufa akiwa katika nyumba yake Connecticut siku ya Jumatano.

Kissinger amekuwa akijishughulisha katika umri wake wa miaka mia moja, akihudhuria mikutano katika Ikulu ya Marekani White House, akichapisha vitabu kuhusu aina ya utawala, na kutoa ushahidi mbele ya kamati ya bunge la Senate kuhusu tishio la nuklia kutoka Korea Kaskazini.

Mwezi Julai, 2023, alifanya ziara ya kushtukiza Beijing alipokutana na rais wa China Xi Jinping.

Mwaka 1970s, alichangia kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya ulimwengu pindi alipokuwa akihudumu kama waziri wa mambo ya nje wa Marekani chini ya aliyekuwa rais wa wakati huo Richard Nixon.

Jitihada za uhamiaji za wakimbizi wa kiyahudi waliozaliwa Ujerumani zilipelekea kufunguliwa kwa diplomasia ya China, mazungumzo muhimu kati ya Marekani na Sovieti, kuongeza mahusiano kati ya Israeli na majirani zake wa Kiarabu, na Mikataba ya Amani ya Paris na Vietman ya Kaskazini.

Utawala wa Kissinger kama msanifu mkuu wa sera za mambo ya nje za Marekani ilififia baada ya kujiuzulu kwa Nixon mwaka 974.

CHANZO:TRT World
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us