AFRIKA
2 DK KUSOMA
Ali Hassan Mwinyi Rais mstaafu wa Tanzania afariki
Kifo cha Mzee Ali Hassan Mwinyi kimetokea katika Hospitali ya Mzena, Dar es salaam, Tanzania, na amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 98.
Ali Hassan Mwinyi Rais mstaafu wa Tanzania afariki
Rais Ali Hassan Mwinyi. Picha; Vyanzo mbalimbali / Others
29 Februari 2024

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amelihutubia taifa kutoka Ikulu ya Magogoni jijini Dar es Salaam Ahamisi na kutoa taarifa ya kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi

Rais mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi amefariki katika Hospitali ya Mzena Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akilihutubia Taifa kupitia Vyombo mbalimbali vya Habari kuhusu kifo cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kilichotokea katika Hospitali ya Mzena Jijini Dar es salaam alikolazwa kwa matibabu ya Saratani ya Mapafu tarehe 29 Februari 2024.

- Ikulu Mawasiliano

Mwinyi, alikuwa rais wa awamu ya pili wa taifa Hilo la Afrika Mashariki kuanzia mwaka 1985 hadi 1995.

Rais huyo wa zamani pia aliwahi kushikilia nyadhifa mbalimbali za mawaziri, ikiwa ni pamoja na mambo ya Ndani, Afya na Rasilimali za asili.

Mzee Mwinyi alichaguliwa kuwa mrithi wake na Baba wa taifa la Tanzania Mwalimu Julius Nyerere alipostaafu mnamo Oktoba 1985.

Soma zaidi kuhusu

Safari ya Rais Mwinyi kupitia link hii hapa

Safari ya Mzee Mwinyi; Urais ambao hakuutegemea

Safari ya Rais Mwinyi; Changamoto za kiuchumi na kisiasa

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us