AFRIKA
2 DK KUSOMA
Watu 45 wafariki kufuatia ajali ya boti mbili pwani ya Djibouti
Shirika la Uhamiaji, IOM ilisema juhudi za utafutaji na uokoaji zinaendelea, huku manusura 32 wakiokolewa.
Watu 45 wafariki kufuatia ajali ya boti mbili pwani ya Djibouti
Vivuko hatari vya baharini kati ya Yemen na Pembe ya Afrika vimeendelea kuwa njia ya wahamiaji wanaokimbia migogoro na matatizo. / Picha: AP / Others
2 Oktoba 2024

Ajali mbili za meli kwenye pwani ya Djibouti zimesababisha vifo vya wahamiaji 45, huku wengi wao wakiwa hawajulikani waliko, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumanne na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).

"Ajali mbili za meli katika pwani ya Djibouti zimesababisha vifo vya wahamiaji 45, na wengi wao bado hawajulikani walipo," msemaji wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) aliandika X.

IOM ilisema juhudi za utafutaji na uokoaji zinaendelea, huku manusura 32 wakiokolewa.

Boti hizo ziliondoka Yemen ikiwa na watu 310 lakini zilipinduka katika Ghuba ya Aden.

Wanakimbia migogoro

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa lilibainisha kuwa linafanya kazi na huduma za dharura za jimbo la Djibouti kuwatafuta abiria waliosalia huku likiwasaidia manusura.

Vivuko hatari vya baharini kati ya Yemen na Pembe ya Afrika vinaendelea kuwa njia ya wahamiaji wanaokimbia migogoro na matatizo, licha ya hatari zinazohusika.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us