20 Juni 2025
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania imesema serikali ya nchi hiyo inachukua hatua za haraka ili kuhakikisha raia wake waliopo nchini Iran na Israel wanarudishwa nchini mwao wakiwa salama.
Taarifa ya Wizara inaonyesha kuwa kuna jumla ya Watanzania 168 katika maeneo mbalimbali nchini Iran, baadhi yao wakiwa ni wanafunzi.
Huku nchini Israel idadi ya Watanzania inakadiriwa kufikia 200 pamoja na watumishi wa Ubalozi wa Tanzania.