Mahakama nchini Kenya imempata Mkenya Rose Njeri na hatia ya kuingilia mifumo ya kompyuta kinyume na kifungu cha 16 cha sheria ya matumizi mabaya ya kompyuta na uhalifu wa mtandaoni namba 5 ya mwaka 2018.
Mahakama ilimwachilia kwa dhamana ya dola 770 (Shilingi 100,000) Rose Njeri hadi Juni 20, 2025, wakati itakapoamua iwapo mashtaka ya uhalifu wa mtandaoni dhidi yake ni halali.
Njeri, aliunda tovuti ya kuruhusu Wakenya kutoa maoni yao kuhusu Mswada wa Fedha wa 2025.
Mahakama imemshtaki kwa kuingilia mfumo wa kompyuta bila kibali, na kuunda programu iliyotuma barua pepe nyingi kwa anwani ya Kamati ya Bunge kuhusu Fedha na kuzituma.
Njeri alifikishwa mahakamani Jumanne akiwakilishwa na wanasheria waliojumuisha Jaji Mkuu mstaafu David Maraga.
Upande wa utetezi uliitaka mahakama kutupilia mbali mashtaka chini ya Sheria ya Matumizi Mabaya ya Kompyuta na Uhalifu wa Mtandaoni, ukisema kuwa Njeri anatumia haki yake ya kikatiba ya uhuru wa kujieleza na kushiriki katika masuala yanayohusu umma.
Jaji Maraga alieleza wasiwasi kuhusu mwenendo wa kuwashtaki raia kwa kushiriki katika masuala ya raia.
Upande wa utetezi pia uliongeza muda wa kuzuiliwa kwa Njeri- siku ya Ijumaa kabla ya sikukuu ya kitaifa- kama sababu inayoweza kuathiri upatikanaji wa haki.
“Kumuweka kizuizini kwa ajili ya kukuza ushirikiano wa umma si tu ni kinyume cha sheria, lakini pia ni mfano hatari dhidi ya ubunifu wa raia na uzingatiaji wa katiba,” Justin Muturi aliyekuwa Mwanasheria Mkuu na Waziri wa masuala ya Umma amesema katika akaunti yake ya X.