AFRIKA
2 dk kusoma
Kesi dhidi ya raia wa Rwanda kuhusu mauaji ya kimbari 'imekwama'
Tangu kukamatwa kwake nchini Afrika Kusini mwezi Mei 2023, Fulgence Kayishema, mmoja wa watoro wanaosakwa sana katika mauaji ya halaiki kwa takriban miongo mitatu, bado hajahukumiwa.
Kesi dhidi ya raia wa Rwanda kuhusu mauaji ya kimbari 'imekwama'
Mshukiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda Fulgence Kayishema REUTERS/Nic Bothma
13 Juni 2025

Mahakama ya Umoja wa Mataifa, International Residual Mechanism for the Criminal Tribunals (IRMCT) imesema kuwa kesi ya Fulgence Kayishema, raia wa Rwanda ambaye anashukiwa kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 dhidi ya Watutsi, inaonekana kukwama.

Tangu kukamatwa kwake nchini Afrika Kusini mwezi Mei 2023, Kayishema, mmoja wa watoro wanaosakwa sana katika mauaji ya halaiki kwa takriban miongo mitatu, bado hajahukumiwa.

Nchini Afrika Kusini, Kayishema, 64, pia anakabiliwa na mashtaka mengi yanayohusiana na ulaghai na ukiukaji wa sheria za uhamiaji za ndani.

"Nchini Afrika Kusini, mambo yanasalia kama yalivyokuwa miaka miwili iliyopita," Serge Brammertz, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa mahakama hiyo ya UN, IRMCT aliliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatano, Juni 11, wakati wa kikao kuhusu shughuli za utaratibu huo.

"Tangu alipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 15 Agosti 2023, kesi hiyo imeahirishwa mara kwa mara, hivi majuzi hadi tarehe 30 Julai 2025."

Alibainisha kuwa ni lazima Kayishema afikishwe mahakamani kwa madai ya uhalifu wake.

Alisema mtuhumiwa huyo wa mauaji ya kimbari anatakiwa kuhamishiwa hadi kituo cha IRMCT kilichopo Arusha, Tanzania na kutoka hapo atahamishiwa hadi Rwanda.

"Waathiriwa na walionusurika wamesubiri zaidi ya miaka 31 sasa. Hawapaswi kusubiri tena," alisema Brammertz.

"Afrika Kusini inapaswa kutekeleza mara moja Hati ya Kukamatwa kwa Utaratibu na kumhamisha Kayishema chini ya ulinzi wa mfumo wa sheria. Ikiwa haiwezi kufanya hivyo, inawajibika chini ya Mkataba wa Mauaji ya Kimbari kumshtaki Kayishema katika mahakama zake."

Mahakama ya IRMCT ilichukua mamlaka ya Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), ambayo ilifungwa mwaka wa 2015.

Washukiwa wawili wa mauaji ya kimbari, Felicien Kabuga na Fulgence Kayishema, walikamatwa Mei 2020 na Mei 2023, mtawalia.

Mnamo Mei 2024, IRMCT ilithibitisha wanaume wawili wa mwisho kati ya watu 93 waliofunguliwa mashtaka kwa kuhusika kwa kuhusika kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda, walikufa.

CHANZO:TRT Afrika and agencies
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us