18 Juni 2025
Mwamuzi huyo mwenye umri wa 42 alisimamishwa na Shirikisho hilo mwezi Novemba 2024 baada ya video kumuonesha akitoa matamshi ya kejeli kuhusu kocha huyo raia wa Ujerumani na timu ya Liverpool.
Coote alifutwa kazi mwezi mmoja baadaye kufuatia "uchunguzi wa kina" kuhusu mienendo yake.
Shirikisho la Soka limemshtaki Coote kukiuka sheria ya bodi hiyo, ya kuwa na mienendo yasiyo na nidhamu na kutumia lugha ya matusi.
Shirikisho linasema alizungumzia kuhusu uraia wa Klopp katika video hiyo ambayo linasema ulikuwa "ukiukwaji mkubwa" wa maadili.
Hata hivyo, Coote aliondolewa madai ya kujihusisha na kamari wakati mwamuzi huyo alipozungumzia kumuonesha kadi ya njano mchezaji mmoja kabla ya mechi kuanza.