ULIMWENGU
2 DK KUSOMA
China yafanya mazoezi ya kijeshi  'kuizunguka' Taiwan
Marekani imetuma chombo cha kuangamiza kombora cha USS Milius kupitia sehemu zinazogombaniwa za Bahari ya China Kusini, na kuibua hasira kutoka kwa China, ambayo ilisema meli hiyo "imeingia kinyume cha sheria" katika eneo lake la maji
China yafanya mazoezi ya kijeshi  'kuizunguka' Taiwan
Mazoezi ya kivita / Photo: AP
10 Aprili 2023

China imeigiza "kuifunga" Taiwan wakati wa siku ya tatu ya mazoezi ya kivita kuzunguka kisiwa hicho kinacho jitawala chenyewe, huku Marekani ikipeleka maangamizi katika maji yanayo daiwa kuwa ya Beijing ili kuonyesha nguvu.

Baada ya siku mbili za mazoezi ambayo ni pamoja na kuonyesha mashambulizi yaliyo lengwa dhidi ya Taiwan na kuzunguka kisiwa hicho, jeshi la China lilisema Jumatatu kwamba michezo ya kivita pia ni pamoja na "kuifunga".

Moja ya kombora la china ambalo pia linabeba ndege lilishiriki katika "mazoezi hayo ya kijeshi", jeshi lilisema.

China ilizindua mazoezi hayo kumjibu Rais wa Taiwan Tsai Ing-wen wiki iliyopita alipokutana na spika wa bunge la Marekani Kevin McCarthy, mkutano ambao ulitarajiwa ungezua jibu la hasira.

Marekani, ambayo mara kwa mara iliitaka China kujizuia, siku ya Jumatatu ilituma chombo cha kuangamiza makombora cha USS Milius kupitia sehemu zinazo gombaniwa za Bahari ya China Kusini.

CHANZO:TRT World
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us