Mahujaji wa Kiislamu wanatekeleza ibada kuu ya mwisho ya Hija, wakirusha mawe kwenye nguzo tatu zinazoashirika uwepo wa shetani katika bonde la Mina karibu na mji wa Makkah, wakati sherehe za Eid al-Adha zikianza kote ulimwenguni.
Ibada hii, inayojulikana kama 'kurusha mawe kwa shetani', inaashiria jinsi Nabii Ibrahim alivyokataa majaribu ya shetani ya kumshawishi asifuate amri ya Mwenyezi Mungu.
Zaidi ya mahujaji milioni 1.6 walitarajiwa kushiriki katika tendo hili la mfano alfajiri ya Ijumaa, kila mmoja akirusha mawe saba kwenye kuta tatu za saruji huko Mina.
Mamlaka Kuu ya Takwimu ya Saudi ilitangaza kuwa mahujaji 1,673,230 walishiriki katika Hija ya mwaka 2025. Kati ya hawa, 1,506,576 walitoka nje ya nchi, huku 166,654 wakiwa ni mahujaji wa ndani, wakiwemo raia wa Saudi na wakaazi.
Nguzo tatu za Jamarat, ambazo mahujaji hurusha mawe, zinawakilisha shetani. Ilikuwa hapa ambapo shetani (shaytan) alimjaribu Nabii Ibrahim.
Vikosi vya usalama vya Saudi vilionekana vikidhibiti umati wa mahujaji wa walipowasili Jabal al-Rahmah, inayojulikana pia kama Mlima Arafat, wakati wa Hija ya kila mwaka.
Mahujaji waliunganisha sala za Magharibi na Isha wakati wa sala ya Isha na kuekea Muzdalifah waqf kwa kufanya Jam' al-takhir.
Hizi ni baadhi ya picha za mahujaji wakati wa Hajj: