25 Juni 2025
Kwa ushindi huo wa Benfica inamaanisha timu hiyo ya Ureno itacheza dhidi ya Cheslea ambayo imemaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi D.
Bayern ilikuwa tayari imeshafuzu baada ya vijana hao wa Vincent Kompany kuwafunga Boca Juniors ya Argentina siku ya Ijumaa 2-1
Katika kipindi cha pili Bayern walikuwa na makali zaidi wakati mkwaju wa Aleksandar Pavlovic ulipookolewa na Leroy Sane akakosa nafasi mbili za wazi, na hawakupata fursa ya kusawazisha goli hilo la pekee na hivyo kumaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo.
Bayern sasa inaelekea Miami kucheza mechi yake dhidi ya timu ya Brazil Flamengo, huku kukiwa na uwezekano wa kucheza robo fainali na mabingwa wa bara Ulaya Paris Saint-Germain iwapo wote watafuzu.