MICHEZO
1 dk kusoma
Manchester City yaifunga Juventus huku Real Madrid ikifuzu hatua ya mtoano
Vijana wa Pep Guardiola Manchester City walionesha uwezo wao katika kombe la dunia la klabu kwa kuwafunga Juventus 5-2 Alhamisi huku Real Madrid ikiishinda Salzburg 3-0 na kufuzu kwa hatua ya mtoano.
Manchester City yaifunga Juventus huku Real Madrid ikifuzu hatua ya mtoano
Manchester City dhidi ya Juventus. / Reuters
27 Juni 2025

Al Hilal wa Saudi Arabia iliifunga Pachuca ya Mexico 2-0, huku Al Ain ikipambana na kuwashinda Wydad Casablanca kwa magoli 2-1.

City ndiyo timu pekee ambayo imeshinda mechi zake zote tatu za kundi lao na kuwapa Juventus wakati mgumu katika uwanja wa Camping huko Orlando.

City sasa watakabiliana na Al Hilal, timu pekee kutoka bara Asia ambayo imefuzu kwa hatua ya mtoano baada ya magoli kutoka kwa Salem Al-Dawsari na Mbrazil Marcos Leonardo dhidi ya Pachuca.

CHANZO:TRT Afrika and agencies
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us