27 Juni 2025
Al Hilal wa Saudi Arabia iliifunga Pachuca ya Mexico 2-0, huku Al Ain ikipambana na kuwashinda Wydad Casablanca kwa magoli 2-1.
City ndiyo timu pekee ambayo imeshinda mechi zake zote tatu za kundi lao na kuwapa Juventus wakati mgumu katika uwanja wa Camping huko Orlando.
City sasa watakabiliana na Al Hilal, timu pekee kutoka bara Asia ambayo imefuzu kwa hatua ya mtoano baada ya magoli kutoka kwa Salem Al-Dawsari na Mbrazil Marcos Leonardo dhidi ya Pachuca.