Uturuki imetuma salamu za rambirambi kwa wahanga wa mafuriko makubwa katika Jimbo la Niger nchini Nigeria.
"Tumehuzunishwa sana na kupoteza maisha na uharibifu uliosababishwa na mafuriko makubwa katika eneo la Mokwa katika jimbo la Niger, Nigeria," Wizara ya Mambo ya Nje ilisema katika taarifa yake Jumamosi.
"Tunatuma rambirambi zetu kwa familia za waliopoteza maisha na kwa watu wa Nigeria," iliongeza.
Idadi ya vifo kutokana na mafuriko makubwa huko Mokwa, kaskazini-kati mwa Jimbo la Niger, imepanda hadi zaidi ya 150, kulingana na taarifa kutoka kwa mamlaka.
Mvua imeleta uharibifu
"Idadi ya sasa ya vifo ni 151," Ibrahim Hussaini, msemaji wa Wakala wa Usimamizi wa Dharura wa Jimbo la Niger (NSEMA), alisema kufuatia mvua kubwa iliyonyesha Jumatano jioni na kuendelea hadi Alhamisi.
Alisema jumla ya watu 3,018 wamekimbia makazi yao, kaya 503 na nyumba 265 zilizokumbwa na maafa hayo. Jamii tatu zimesombwa na maji.
Mvua hiyo imesababisha uharibifu mkubwa na kusomba nyumba na miundombinu ikiwemo barabara na madaraja mawili.