MICHEZO
1 dk kusoma
Xabi Alonso ameteuliwa kuwa meneja wa Real Madrid kwa mkataba wa miaka 3
Mchezaji mwenye umri wa miaka 43 atatambulishwa Jumatatu kama meneja mpya katika hafla itakayofanyika Real Madrid City
Xabi Alonso ameteuliwa kuwa meneja wa Real Madrid kwa mkataba wa miaka 3
Xabi Alonso atatambulishwa kama meneja Mpya wa Real Madrid Jumatatu Mei 26 / AA
25 Mei 2025

Real Madrid C. F. ilithibitisha Jumapili kwamba Xabi Alonso atakuwa kocha wao mkuu kwa misimu mitatu ijayo.

"Xabi Alonso alianza maisha yake ya ukocha katika chuo cha mafunzo ya soka ya Real Madrid, akichukua mikoba ya Vijana wa U-12 kwa kampeni ya 2018-2019 na kushinda ligi na Torneo de Campeones," Real Madrid ilisema katika taarifa.

"Sasa anarejea Real Madrid kama mmoja wa makocha bora zaidi duniani baada ya kuweka historia katika klabu ya Bayer Leverkusen, ambako alishinda ligi, kombe na Kombe la Super Cup la Ujerumani kwa misimu mitatu," iliongeza.

Klabu hiyo iliongeza kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 43 atatambulishwa Jumatatu kama kocha mkuu mpya katika hafla itakayofanyika katika majengo ya Real Madrid City.

CHANZO:AA
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us