AFRIKA
2 dk kusoma
Helikopta ya walinda amani wa Umoja wa Afrika yapata ajali uwanja wa ndege Somalia
Wafanyakazi wa uokoaji na zimamoto wamefika katika uwanja wa ndege wa Aden Adde mjini Mogadishu na kuzima moto kutokana na ajali ya helikopta
Helikopta ya walinda amani wa Umoja wa Afrika yapata ajali uwanja wa ndege Somalia
Moshi ukionekana upande wa uwanja wa ndege wa Aden Adde mjini Mogadishu, Somalia 2 Julai, 2025 / Reuters
2 Julai 2025

Helikopta ya vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika nchini Somalia ilianguka siku ya Jumatano katika uwanja wa kimataifa wa ndege katika mji mkuu,Mogadishu, afisa mmoja alisema.

Afisa wa sekta ya usafiri wa ndege mjini Mogadishu, ambaye hakutaka kutambulishwa kutokana na kutoruhusiwa kuzungumza na vyombo vya habari, ameliambia shirika la Anadolu kuwa helikopta hiyo ya walinda amani ilikuwa na maafisa wanane na ililazimika kutuwa kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Aden Adde mjini Mogadishu baada ya kuondoka uwanja wa Balidoogle ambapo kuna wanajeshi wa Marekani na Somalia.

Alisema kuwa kuna watu waliofariki bila kutaja idadi ya waliouawa au waliojeruhiwa kwenye ajali hiyo, lakini akaongeza kuwa maafisa wa uokoaji na zimamoto walifika kwenye eneo hilo na kuuzima moto wa helikopta iliyopata ajali.

AUSSOM ina wanajeshi 11,000 nchini Somalia kusaidia jeshi la nchi hiyo kukabiliana na wapiganaji wa kundi la al-Shabaab.

Moshi mkubwa

Vikosi hivyo vinajumuisha wanajeshi kutoka nchi ya Uganda na Kenya.

Halima Ahmed, mkazi wa wilaya ya Wabari mjini Mogadishu aliyezungumza na Anadolu kwa njia ya simu, amesema aliona moshi mkubwa kutoka upande wa uwanja wa ndege siku ya Jumatano.

Ndege kadhaa zilichelewa kupaa na kutuwa kutokana na tukio hilo lakini kwa sasa hali inasemekana kurudi kama kawaida.

CHANZO:AA
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us