ULIMWENGU
1 dk kusoma
Israeli yashambulia maeneo ya ‘jeshi na nuklia’ ya Iran, na kumuua mkuu wa jeshi na kiongozi wa IRGC
Sauti za mlipuko zilisikika katika mji wa Tehran na maeneo mengine huku Israeli ikimuua kiongozi wa jeshi wa Iran Mohammad Bagheri na mkuu wa kikosi cha mapinduzi Hossein Salami, imeripoti televisheni ya taifa.
Israeli yashambulia maeneo ya ‘jeshi na nuklia’ ya Iran, na kumuua mkuu wa jeshi na kiongozi wa IRGC
Israeli imesema inatarajia mashambulizi ya makombora katika "siku za hivi karibuni". / Reuters
13 Juni 2025

Israeli imeanzisha mashambulizi katika kile inachosema “maeneo ya nuklia na jeshi” ya Iran, huku vyombo vya habari za Iran vikiripoti kuwepo kwa milipuko katika mji mkuu wa Tehran, na kutangaza kuuawa kwa kiongozi wa jeshi Mohammad Bagheri na kiongozi wa kikosi cha mapinduzi Hossein Salami.

“Meja Jenerali Mohammad Bagheri, mkuu wa majeshi ameuliwa shahidi,” limesema shirika la utangazaji.

Bagheri, aliyeuliwa katika shambulio la siku ya Ijumaa, ameongoza jeshi la Iran tangu 2016, alionekana kama msanifu katika mpango wa makombora wa Iran.

Na Salami alionekana kama mtu muhimu katika uongozi wa jeshi la Iran na mmoja wa makamanda muhimu katika kikosi cha wanajeshi wa mapinduzi IRGC.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us