UTURUKI
1 dk kusoma
Baghladesh yatafuta msaada Uturuki kurudisha misitu, na kuhifadhi mazingira
Dhaka inatafuta msaada wa kitaalamu wa Uturuki katika kudumisha utalii na uhifadhi wa mazingira baada ya kupoteza wanyama pori. Ankara imeonyesha utayari wa kusaidia katika mradi wa pamoja kupitia Shirika lake la Maendeleo TIKA.
Baghladesh yatafuta msaada Uturuki kurudisha misitu, na kuhifadhi mazingira
Mshauri wa mazingira katika serikali ya mpito, Syeda Rizwana Hasan, ameonyesha nia yake katika mkutano wa Jumanne na Balozi wa Uturuki Bangladesh Ramis Sen katika ofisi yake Dhaka, imesema taarifa ya Waziri wa Mazingira. / TRT World
27 Mei 2025

Bangladesh inatafuta msaada wa kiufundi kutoka Uturuki katika kurudisha misitu na maendeleo endelevu ya utalii, ikilenga kunufaika kutoka uzoefu wa Ankara katika utalii wa kuhifadhi mazingira.

Mshauri wa mazingira katika serikali ya mpito, Syeda Rizwana Hasan, ameonyesha nia yake katika mkutano wa Jumanne na Balozi wa Uturuki Bangladesh Ramis Sen katika ofisi yake Dhaka, imesema taarifa ya Waziri wa Mazingira.

Hasan ameonyesha umuhimu wa kushirikisha wataalamu katika kuhifadhi maeneo ya misitu yaliyoathiriwa na migogoro ya binadamu na wanyama pori.  Amesisitiza umuhimu wa kutumia aina ya miti sahihi na kufuata nyenzo ambazo zitalinda mazingira.

Akigusia tukio la hivi karibuni ambalo lilihusisha vifo vya tembo kadhaa kutokana na uharibifu wa mazingira na uhaba wa chakula, amesema jitihada za kurudisha mazingira ni muhimu kuepusha uharibifu zaidi.

Hasan pia, ameelezea mipango wa eneo la Sylhet mashariki mwa Bangladesh, unaolenga kukuza utalii endelevu utakaokuwa na athari ndogo kwa mazingira.

Balozi Sen amekaribisha pendekezo na kusema Shirika la Ushirikiano na Uratibu la Uturuki (TIKA) liko tayari kuunga mkono miradi ya pamoja ya kiwango cha kati ya pamoja.

Ameahidi kuiunganisha ofisi ya mshauri na idara husika za Uturuki ili kupitia fursa za miradi na kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us