Umoja wa Mataifa umetoa ripoti ya nchi zenye furaha zaidi duniani, wakati ulimwengu ukiwa unaadhimisha siku ya kimataifa ya furaha, Machi 20.
Katika ripoti hiyo iliyotolewa siku ya Jumatano, Libya ndiye kinara wa furaha zaidi Afrika.
Nchi hiyo ilifuatiwa na Mauritius na Afrika Kusini, wakati Lesotho ilikuwa ya mwisho kwa kuwa na furaha, kwa upande wa bara la Afrika.
Finland ilishika nafasi ya kwanza ikifuatiwa kwa karibu na Denmark, Iceland na Sweden, wakati nchi nane kutoka Afrika ziliambulia nafasi kumi za mwisho katika orodha hiyo.
Maisha bora zaidi
Raia kutoka nchi 143 duniani waliombwa kutoa tathmini ya maisha yao kutoka kiwango cha 0 mpaka 10, huku 10 ikiwakilisha maisha bora.
Matokeo kutoka miaka mitatu yametengezewa wastani na hatimaye kuwepo na orodha hiyo.
Jambo la kufurahisha zaidi ni kuona namna vijana wengi, haswa kutoka ukanda wa kusini mwa jangwa la Sahara wakiridhika na maisha, ingawa hali ya maisha yao ilikuwa ya chini.
Ripoti hiyo, ambayo hutolewa kila mwaka, ilianzishwa mwaka 2012 na Umoja wa Mataifa, kupitia malengo endelevu ya maendeleo.
Nchi 10 za Afrika zenye furaha zaidi kulingana na ripoti hiyo
66 - Libya
70 - Mauritius
83 - Afrika Kusini
85 - Algeria
89 - Congo Brazzaville (Jamhuri ya Congo)
90 - Msumbiji
95 -Gabon
96 - Ivory Coast
97 - Guinea
99 - Senegal
Nchi zingine za Afrika :
102 - Nigeria
104 - Cameroon
107 - Morocco
109 - Niger
110 - Burkina Faso
114 - Kenya
120 - Ghana
127 - Egypt
130 - Ethiopia
Nchi 10 zisizo na furaha:
131 - Tanzania
132 - Visiwa vya Komoro
134 - Zambia
135 - Eswatini
136 - Malawi
137 - Botswana
138 - Zimbabwe
139 - Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
140 - Sierra Leone
141 - Lesotho
Ripoti hiyo pia imetumia vigezo mbali mbali vikiwemo kipato, afya, ukarimu, kukosekana kwa rushwa na msaada wa kijamii.