ULIMWENGU
1 dk kusoma
Kremlin yasema bado hakuna mpango wa mazungumzo ya simu kati ya Putin na Trump
Kremlin imesema bado hakuna mpango wa mazungumzo kwa njia ya simu kati ya Putin na Trump.
Kremlin yasema bado hakuna mpango wa mazungumzo ya simu kati ya Putin na Trump
Rais wa Urusi Vladimir Putin / AP
29 Mei 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin bado hajakuwa na mpango wa kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Marekani Donald Trump, msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema Alhamisi.

Trump hivi karibuni ameonyesha kughadhibishwa na Putin, huku akionya siku ya Jumanne kwamba kiongozi huyo wa Urusi alikuwa “anachezea moto” kwa kukataa kushiriki mazungumzo ya kusitisha mapigano na Kyiv huku vikosi vyake vikiendelea kufanya mashambulizi.

Katika majibu yake kwa kauli ya Trump, Kremlin imesema Jumatano kwamba Rais Putin anaweka mbele maslahi ya taifa la Urusi kuliko kitu chochote.

Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us