29 Mei 2025
Rais wa Urusi Vladimir Putin bado hajakuwa na mpango wa kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Marekani Donald Trump, msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema Alhamisi.
Trump hivi karibuni ameonyesha kughadhibishwa na Putin, huku akionya siku ya Jumanne kwamba kiongozi huyo wa Urusi alikuwa “anachezea moto” kwa kukataa kushiriki mazungumzo ya kusitisha mapigano na Kyiv huku vikosi vyake vikiendelea kufanya mashambulizi.
Katika majibu yake kwa kauli ya Trump, Kremlin imesema Jumatano kwamba Rais Putin anaweka mbele maslahi ya taifa la Urusi kuliko kitu chochote.