AFRIKA
1 dk kusoma
Omar al-Mukhtar: Shujaa wa Uhuru wa Libya
Omar al-Mukhtar: Shujaa wa Uhuru wa Libya / TRT Afrika Swahili
21 Aprili 2025

Alizaliwa mwaka 1860 kijijini Zawiyat Janfur, Omar al-Mukhtar alikua mwalimu wa Kiislamu na kiongozi wa mapambano dhidi ya ukoloni wa Italia.

Kwa zaidi ya miaka 20, aliiongoza vita ya msituni dhidi ya majeshi ya Italia — akiwa na maarifa ya kina ya ardhi ya Cyrenaica na moyo wa kujitolea kwa ajili ya uhuru wa Libya.

Alikamatwa Septemba 1931, akahukumiwa na kunyongwa — lakini hadhi yake ilizidi kuwa ya shujaa wa taifa.

Leo, al-Mukhtar ni alama ya kupinga dhulma na ukoloni. Historia yake haijafutika.

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us