21 Aprili 2025
Alizaliwa mwaka 1860 kijijini Zawiyat Janfur, Omar al-Mukhtar alikua mwalimu wa Kiislamu na kiongozi wa mapambano dhidi ya ukoloni wa Italia.
⠀
Kwa zaidi ya miaka 20, aliiongoza vita ya msituni dhidi ya majeshi ya Italia — akiwa na maarifa ya kina ya ardhi ya Cyrenaica na moyo wa kujitolea kwa ajili ya uhuru wa Libya.
⠀
Alikamatwa Septemba 1931, akahukumiwa na kunyongwa — lakini hadhi yake ilizidi kuwa ya shujaa wa taifa.
⠀
Leo, al-Mukhtar ni alama ya kupinga dhulma na ukoloni. Historia yake haijafutika.