4 Julai 2025
Baada ya kupata matokeo ambayo wengi hawakutarajia kwenye hatua ya mtoano ya timu 16 katika Kombe la Dunia la Klabu, timu ya Saudi Arabia ya Al-Hilal sasa inaangazia hatua ya nusu fainali wakati itakapokabiliana na Fluminense ya Brazil huko Orlando siku ya Ijumaa.
Timu hiyo inayocheza kwenye Ligi Kuu ya Saudia ya Saudi Pro League iliwashangaza wababe wa Ligi Kuu ya England Manchester City kwa kuwafunga 4-3 katika hatua ya timu 16.
Wakati huo Al-Hilal walionesha ujasiri na ari kubwa dhidi ya vijana wa Pep Guardiola, wakiimarika kwa ujuzi na ubunifu.
Pamoja na kuwa itaingia katika kumbukumbu kama jambo kubwa kwa klabu kutoka Mashariki ya Kati, ushindi huo ulichangiwa zaidi na wachezaji wa kimataifa.