Rais wa Marekani Donald Trump amepinga mpango wa Israel wa kumuua kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei, afisa mkuu wa Marekani ameliambia shirika la habari la AFP.
"Tuligundua kwamba Waisraeli walikuwa na mipango ya kumpiga kiongozi mkuu wa Iran. Rais Trump alikuwa kinyume na hilo na tuliwaambia Waisraeli wasifanye hivyo," afisa huyo wa Marekani alisema Jumapili, akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina.
"Sitazungumzia katika hilo," aliiambia Fox News.
"Lakini naweza kukuambia,... tutafanya kile tunachohitaji kufanya, na nadhani Marekani inajua ni nini kizuri kwa Marekani," alisema.
Njama ya muda mrefu
Matamshi hayo yalikuja wakati Israel na Iran zikibadilishana safu nyingine ya makombora siku ya Jumapili, huku wakaazi wakiambiwa watafute makazi huku milipuko ikisikika juu ya Jerusalem, na mifumo ya ulinzi wa angani ikiripotiwa kuwashwa mjini Tehran.
Baada ya miongo kadhaa ya uadui na vita vya muda mrefu vilivyopiganwa kupitia washirika na operesheni za siri, mzozo wa hivi karibuni uliashiria mara ya kwanza kwa nchi hizo kubadilishana makombora kwa nguvu kama hiyo, na kusababisha hofu ya mzozo mrefu ambao unaweza kukumba Mashariki ya Kati nzima.
Ilianza siku ya Ijumaa, wakati Israel ilipoanzisha mashambulizi ambayo yaliwaua makamanda wakuu wa kijeshi na wanasayansi wa nyuklia, na kushambulia kambi za kijeshi, maeneo ya nyuklia na maeneo ya makazi kote nchini.
Shambulio la Tel Aviv bila sababu lilisababisha mzozo huo, na kuifanya Iran kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya Israel.
Marekani haihusiki kwa wakati huu
Mashambulizi na majibu ya mashambulio yameendelea tangu wakati huo.
Netanyahu pia alipendekeza vikali kwa Fox News kwamba Israeli ilimuua mkuu wa kijasusi wa Iran Mohammad Kazemi, akisema hivi karibuni "imempata afisa mkuu wa upelelezi na naibu wake huko Tehran" wakati ndege zake zilifanya uvamizi katika mji mkuu.
Trump amesisitiza kuwa Washington, mshirika mkubwa wa Israel "haina uhusiano wowote" na kampeni ya Israel ya kulipua mabomu.
Rais wa Marekani alisisitiza kwa ABC News Jumapili kwamba Marekani "haihusiki kwa wakati huu" katika harakati za kijeshi.
Pia alisema atakuwa "wazi" kwa mwenzake wa Urusi Vladimir Putin kuwa mpatanishi wa kutatua mzozo huo.