Masoko ya kimataifa yanafuatilia kwa karibu Mlango-Bahari wa Hormuz, ukanda muhimu wa mafuta na gesi( LNG) kusafirishwa duniani, huku kukiwa na hofu kwamba mzozo unaoongezeka kati ya Israel na Iran unaweza kuvuruga trafiki kupitia njia hiyo nyembamba ya maji.
Mlango wa bahari wa Hormuz ni njia nyembamba lakini muhimu ya baharini ambayo takriban theluthi moja ya biashara ya mafuta duniani, inayochukua mapipa milioni 17 hadi 20 ya mafuta ghafi hupitia kila siku.
Takriban asilimia 70 ya kiasi cha mafuta huenda Asia kupitia njia hii, huku China, Japan, India, Korea Kusini, Singapore, Thailand, Pakistan na Ufilipino zikiwa miongoni mwa wapokeaji wakubwa, kulingana na Shirika la Kimataifa la Nishati.
Njia hiyo pia ni muhimu kwa mauzo ya gesi ya LNG, hasa kutoka Qatar na Falme za Kiarabu, ambayo inachangia asilimia 20 ya biashara ya kimataifa ya gesi.
Ulaya ni kituo kikuu cha LNG ambacho hupitia Hormuz.
Ijapokuwa Iran iliwahi kutishia kufunga barabara hiyo ili kukabiliana na mvutano wa kisiasa wa kijiografia, bado haijachukua hatua juu ya vitisho kama hivyo.
Walakini, matarajio ya mzozo mpana wa kikanda kufuatia mashambulio ya anga ya Israeli dhidi ya Iran yameongeza wasiwasi juu ya uwezekano wa usumbufu wa usambazaji na kupanda kwa bei ya nishati.
Shirika la Operesheni za Biashara ya Bahari la Uingereza (UKMTO) lilisema Jumatano kwamba kuongezeka kwa mvutano katika eneo hilo kunaweza kuzidisha shughuli za kijeshi katika njia muhimu za majini na kuathiri usafiri wa baharini, wakati Baraza la Baltic na Kimataifa la Bahari pia lilionya kwamba shambulio lolote linaweza kuathiri moja kwa moja usafiri wa baharini.