AFRIKA
1 dk kusoma
Tanzania: Chama cha CCM kufanya mchakato wa uteuzi wa wagombea ubunge, viti maalumu
Tanzania itafanya Uchaguzi Mkuu ambao utahusisha mchakato wa kumchagua rais, wabunge, madiwani na wajumbe wa baraza la wawakilishi, Oktoba 29, 2025.
Tanzania: Chama cha CCM kufanya mchakato wa uteuzi wa wagombea ubunge, viti maalumu
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, anayeshughulikia itikadi, uenezi na mafunzo Amos Makalla./Picha:@ccm_tanzania
20 Agosti 2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha nchini Tanzania, kitafanya kikao cha siku mbili chenye lengo la kufanya teuzi za Wagombea Ubunge, wa Bunge la nchi hiyo, wabunge wa Viti Maalumu, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Viti Maalum.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, anayeshughulikia itikadi, uenezi na mafunzo Amos Makalla, vikao hivyo ambavyo vitaongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM, vitafanyika Agosti 21 na 23, 2025 jijini Dodoma.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us