tokea masaa 5
Matokeo hayo yameihakikishia Sudan kumaliza kileleni mwa kundi D kwa tofauti ya magoli, huku mabingwa Senegal wakifuzu kwa kumaliza nafasi ya pili.
Wakati huo huo, Nigeria imeifunga Congo 2-0 jijini Dar es Salaam, lakini juhudi hizo za Tai wa Kijani hazikuwasaidia kuwaondoa Sudan na Senegal kwenye nafasi zao.
Ilisemekana kuwa mechi ya maamuzi ya kundi D, na naam ilikuwa kama ilivyotarajiwa, hata bila magoli.
Zilizopendekezwa
Sudan, ambayo inafunzwa na kocha raia wa Ghana Kwesi Appiah, ilikuwa imechangamka sana baada ya kuicharaza Nigeria 4-0.
Senegal, mabingwa wa sasa, walifahamu kuwa iwapo wangeshindwa ina maana wangeyaaga mashindano lakini pia walikuwa na nia ya kumaliza wa kwanza kwenye kundi hilo,ambalo hilo halikutimia.
CHANZO:TRT Afrika Swahili















