AFRIKA
1 dk kusoma
Marekani yaweka sheria kali za viza kwa raia wa Nigeria, yachunguza mitandao ya kijamii ya waombaji
Hii ni sheria ya hivi karibuni ya Marekani huku uongozi wa Trump ukiendeleza ukali dhidi ya wahamiaji, hasa wakilenga nchi za Afrika.
Marekani yaweka sheria kali za viza kwa raia wa Nigeria, yachunguza mitandao ya kijamii ya waombaji
Masharti haya ya sasa hivi yanakuja baada ya Marekani kubadilisha sera yake ya viza inayoathiri raia wa Nigeria. / Wengine
18 Agosti 2025

Marekani imetangaza masharti mapya ya viza kwa raia wa Nigeria, yanayohitaji waombaji wote kuweka wazi akaunti zao za mitandao ya kijamii katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kwa lengo la kufanyiwa mchujo.

‘‘Kutoweka taarifa za mitandao ya kijamii kunaweza kusababisha mtu kunyimwa viza na uwezekano wa kukosa viza katika siku za baadaye,’’ Ubalozi wa Marekani nchini Nigeria ulisema katika taarifa kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu, ukiongeza kuwa wanaotuma maombi ya viza ‘‘wanahitaji kuweka wazi akaunti zao za mitandao yote ya kijamii ambayo wametumia katika kipindi cha miaka 5 iliyopita katika fomu ya maombi ya DS-160.’’

Serikali ya Nigeria bado haijasema lolote kuhusu taarifa hii mpya ya viza za Marekani.

Agizo hili linakuja huku ikiweka masharti makali ya viza zake na kuweka vikwazo vya usafiri kwa nchi kote duniani, hasa kwa mataifa ya Afrika.

Mwezi Julai, Nigeria iliiomba serikali ya Trump kufikiria upya kuhusu vikwazo vya muda uliowekewa raia wake wa Nigeria wa kukaa nchini humo kwa muda usiozidi miezi mitatu. Masharti hayo yameathiri pia mataifa ya Cameroon na Ethiopia.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us