ULIMWENGU
2 dk kusoma
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu hali mbaya Gaza huku kukiwa na vikwazo vya Israel kwa misaada
Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu watu kuondolewa katika makazi yao na kuongezeka kwa vikwazo vya Israel kuhusu kupeleka misaada Gaza.
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu hali mbaya Gaza huku kukiwa na vikwazo vya Israel kwa misaada
Hali kwa watu wa Gaza ni mbaya huku uvamizi wa Israel katika eneo hilo ukitishia maisha ya watu. / Picha: AP
tokea masaa 8

Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuongezeka kwa kuondoka kwa watu katika makazi yao na kuongezeka kwa vikwazo vya Israel kuhusu kupeleka misaada Gaza.

"Wenzetu wanatupa taarifa kuwa watu wanakimbia makazi yao, wakielekea maeneo ya pwani. Tangu Agosti 14, washirika wetu wanatuambia watu wanaondoka na wamepata idadi ya watu wapya zaidi ya 76,000 ambao wanaondoka makazi yao," msemaji Stephane Dujarric alisema katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumanne.

Alieleza kuwa "watu zaidi ya 23,000 kati ya hawa walikuwa wanatoka maeneo ya kaskazini hadi kusini mwa Gaza. Wengi wa walioondoka katika makazi yao wanatoka katika Jimbo la Gaza."

Akinukuu Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Masuala ya Uratibu na Misaada (OCHA), alisema kuwa "maeneo ya pwani katika mji yamejaa watu sana katika mahema, kulazimisha wale wanaokimbia kutoka Gaza City kuelekea maeneo ya kaskazini katika maeneo karibu na Zikim, ingawa maeneo hayo tayari wameonywa kuhusu kuondoka maeneo hayo."

Hali mbaya kwa watu wa Gaza

Dujarric pia alieleza kuhusu hali mbaya inayoongezeka kwa watu, akisema "kumekuwa na taarifa za kila siku na vifo vinavyotokana na utapiamlo Gaza."

Onyo kuhusu vikwazo vinavyoendelea vya Israel kuhusu misaada, alieleza kuwa "makundi ya kutoa misaada yamewekewa vikwazo vingi ndani ya Gaza."

"Kati ya Ijumaa na Jumatatu, ratiba ya misaada mara tatu ilikwamishwa au kukataliwa moja kwa moja na mamlaka za Israel. Ratiba 12 kati ya 37 ambazo tulikuwa nazo na wao ," alisema.

"Matokeo yake, ratiba nyingi zimeshindwa kutimizwa," Dujarric aliongeza, akieleza kuwa "ukaguzi uliokithiri wa mamlaka za Israel unaendelea kuchelewesha ufikishwaji wa misaada" katika bandari ya Ashdod.

CHANZO:AA
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us