AFRIKA
2 dk kusoma
Waasi waliokuwa na mapanga wameua takriban watu 52 mashariki mwa DRC
Waasi wa ADF waliokuwa na mapanga wamewaua takriban raia 52 katika maeneo ya Beni na Lubero mashariki mwa DRC katika siku za hivi karibuni, maafisa wa Umoja wa Mataifa na mashinani walisema Jumatatu.
Waasi waliokuwa na mapanga wameua takriban watu 52 mashariki mwa DRC
Waasi wa ADF, waliokuwa na silaha duni, waliporomosha vijiji mashariki mwa DRC na kuwaua watu zaidi ya 50 katikati ya Agosti 2025. / Picha: AFP
tokea masaa 7

Waasi wa ADF waliokuwa wamejihami kwa mapanga na majembe wamewaua angalau raia 52 katika maeneo ya Beni na Lubero mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika siku za hivi karibuni, maafisa wa Umoja wa Mataifa na wa eneo hilo wamesema.

Waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) walikuwa wakilipa kisasi dhidi ya raia baada ya kushindwa na vikosi vya Congo, alisema Luteni Elongo Kyondwa Marx, msemaji wa jeshi la eneo hilo.

"Walipofika, waliamsha wakazi kwanza, wakawakusanya mahali pamoja, wakawafunga kwa kamba, kisha wakaanza kuwachinja," alisema Macaire Sivikunula, mkuu wa sekta ya Bapere huko Lubero, alipoongea na Reuters mwishoni mwa wiki.

Takriban raia 30 waliuawa katika kijiji cha Melia pekee, alisema Alain Kiwewe, msimamizi wa kijeshi wa eneo la Lubero, alipoongea na Reuters.

Wanawake na watoto miongoni mwa waathiriwa

"Miongoni mwa waathiriwa walikuwemo watoto na wanawake, huku nyumba kadhaa zikichomwa moto," alisema.

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO) ulilaani "kwa maneno makali zaidi" mashambulizi ya ADF kati ya Agosti 9 na 16, msemaji wa ujumbe huo alisema Jumatatu.

Mashambulizi hayo yaliwaua angalau raia 52, wakiwemo wanawake wanane na watoto wawili, na idadi hiyo inaweza kuongezeka kwani juhudi za utafutaji bado zinaendelea, msemaji huyo aliongeza.

ADF ni miongoni mwa makundi kadhaa ya wanamgambo yanayopigania ardhi na rasilimali katika mashariki mwa Kongo yenye utajiri wa madini.

Operesheni dhidi ya ADF

Jeshi la Congo na mshirika wake, Uganda, wameongeza operesheni dhidi ya ADF katika wiki za hivi karibuni.

Mwisho wa Julai, waasi wa ADF waliwaua watu 38 katika shambulio kwenye kanisa mashariki mwa Congo.

CHANZO:Reuters
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us