MICHEZO
1 dk kusoma
Ni Angola au Kenya mechi ya pili kundi A CHAN 2024?
Paa weusi Angola leo wanaingia uwanjani kutafuta ushindi wao wa kwanza wakati watakapokabiliana na Harambee Stars ya Kenya katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.
Ni Angola au Kenya mechi ya pili kundi A CHAN 2024?
Timu ya Taifa ya Angola. / Picha: FAF
7 Agosti 2025

Kocha wa Harambee Stars Benni McCarthy anasema watakuwa makini wakati watakapokabiliana na Angola kwenye mechi ya kundi ya A, huku wakiwa tayari wametia alama tatu kibindoni.

Timu ya Angola, ambayo iko katika nafasi ya 85 katika orodha ya Shirikisho la Soka duniani FIFA, ikilinganishwa na Kenya, ambayo iko katika nafasi ya 109, na inabidi wakabiliane vilivyo kuepuka wasipoteze fursa ya kufuzu kwa hatua ya muondoano.

Ushindi kwa Harambee Stars hakutowapa zawadi ya fedha zaidi ya dola 7,000 kutoka kwa Rais William Ruto lakini kutawasogeza karibu kufuzu kwa hatua nyingine.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us