AFRIKA
1 dk kusoma
Uganda yaingia robo fainali baada ya sare dhidi ya Bafana Bafana
Uganda imeweka historia ya kuingia robo fainali katika mashindano ya CHAN 2024 baada ya sare 3-3 dhidi ya Afrika Kusini mbele ya mashabiki zaidi ya elfu 34 katika uwanja wa Mandela jijini Kampala Jumatatu
Uganda yaingia robo fainali baada ya sare dhidi ya Bafana Bafana
Timu ya Uganda. / Picha: CAF
tokea masaa 9

Kwa matokeo hayo, yakizingatiwa pamoja na ya sare ya sifuri kwa sifuri kwa Algeria dhidi ya Niger kwenye kundi C, imewahakikishia Korongo wa Uganda kumaliza kundi hilo wakiwa kileleni kwa mara ya kwanza katika historia yao ya kucheza mashindano ya CHAN, huku Afrika Kusini ikiyaaga michuano hiyo.

Uganda yaweka Historia Kampala

Walihitaji tu sare ili kuingia hatua ya robo fainali, Uganda ilikuwa na kila sababu ya kuamini hilo baada ya goli la Jude Ssemugabi katika dakika 31.

Kufikia mapumziko Uganda ilikuwa bado na ushindi huo mwembamba, lakini katika kipindi cha pili ilikuwa ni nipe nikupe na wakati mmoja Afrika Kusini ikafika kuongoza mechi hiyo.

Rogers Torach aliwainua mashabiki wa nyumbani alipoingiza goli katika dakika ya 96, na kupata sare waliyoikuwa wakiihitaji.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us