tokea masaa 12
Goli la Ismaël Camara la dakika ya 62 liliwapa Guinea uongozi na wakawa na imani kwa muda mrefu kuwa wanachukua alama zote tatu, lakini Soufiane Bayazid alisawazisha ikiwa imebaki dakika mbili kwa mechi kumalizika na kuendeleza rekodi ya Algeria ya kutofungwa hata mechi moja.
Matokeo haya yamebakisha Guinea ikiwa na alama nne baada ya mechi nne, na matumaini ya kuendelea zaidi ya hatua ya makundi yakiwa na ati ati, huku Algeria ikiwa na alama tano ikiwa bado na nafasi kubwa ya kuingia kwenye robo fainali wakati wakisubiri mechi ya mwisho.
Zilizopendekezwa
Wenyeji Uganda wanaoongoza kundi hilo la C wana alama sita.
Mechi nyingine kwenye kundi hilo kati ya Niger na Afrika Kusini imemalizika kwa sare ya sifuri kwa sifuri.
CHANZO:TRT Afrika Swahili