Waendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, wataanza kuwasilisha ushahidi Jumanne ili kuunga mkono mashtaka yao dhidi ya kiongozi wa waasi wa Uganda Joseph Kony katika kesi ya kwanza kabisa ya kusikilizwa kwa mahakama hiyo ya kimataifa.
Kony, mwanzilishi na kiongozi wa kundi la Lord’s Resistance Army, au LRA, anakabiliwa na shutuma za uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
Mahakama hiyo inayoitwa uthibitisho wa kusikilizwa kwa mashtaka inakuja miongo miwili baada ya kutoa hati ya kukamatwa kwa Kony kwa madai ya uongozi wake wa kundi la kikatili la waasi ambalo lilijulikana kwa ukatili, ikiwa ni pamoja na kuwateka nyara watoto na kuwakata viungo mateka.
Usikilizaji wa kesi mbele ya ICC sio kesi halisi, lakini unaruhusu waendesha mashtaka kuelezea kesi yao mahakamani.
Kony atawakilishwa na wakili wa utetezi bila yeye mwenyewe kuwepo.
Baada ya kupitia ushahidi, majaji wanaweza kutoa uamuzi wa kuthibitisha au kutothibitisha mashtaka dhidi ya Kony, lakini hawezi kuhukumiwa isipokuwa akiwa chini ya ulinzi wa ICC.
Mashtaka dhidi ya Kony
Kony anakabiliwa na mashtaka 39 yakiwemo mauaji, utumwa wa kijinsia, ubakaji, na kuwasajili watoto askari, mashtaka yote yanayodaiwa kufanywa mwaka 2003 na 2004 kaskazini mwa Uganda.
Usikilizaji huo umeonekana kama kesi ya majaribio kwa mahakama kusonga mbele na kesi nyengine ambapo uwezekano wa kuwa na mshukiwa kizuizini unachukuliwa kuwa wa mbali, kama vile Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu.
Kony apata umaarufu duniani mnamo 2012 wakati video kuhusu uhalifu wake iliposambaa.
Licha ya umakini na juhudi za kimataifa za kumkamata, bado yuko huru.
LRA ilianza mashambulizi yake nchini Uganda katika miaka ya 1980, wakati Kony alipotaka kupindua serikali.
Baada ya kusukumwa nje ya Uganda, wanamgambo hao walifanya ugaidi katika vijiji vya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sudan Kusini.
Zaidi walitumia watoto kama askari wake, kukata viungo vya raia na kuwafanya wanawake kuwa watumwa.
Walionusurika wanakaribisha malipo
Kesi ya ICC dhidi ya Kony itafuatiliwa na wengi nchini Uganda, ambapo walionusurika wanakaribisha mashtaka hayo huku wakijutia kushindwa kumkamata.
"Alifanya mambo mengi mabaya," alisema Odong Kajumba, ambaye alitoroka LRA baada ya kukamatwa na kulazimishwa kubeba gunia la sukari hadi mpaka wa Uganda na Sudan mwaka 1996.
Ikiwa wanaweza kumkamata Kony, alisema, "Nina furaha sana."
Sio kila mtu anafurahishwa na mchakato unaoendelea. "Kwa nini unataka kumshtaki mtu usiyempata? Wanapaswa kwanza kumpata," alisema Odonga Otto, mbunge wa zamani kutoka kaskazini mwa Uganda.
"Ni mzaha. Kuleta kesi ya Kony akiwa kizuizini kungefanya kesi za mahakama kuwa na uhalisia zaidi" kwa waathiriwa,” alisema.