Watu wasiopungua 40 wamefariki katika eneo la Darfur, Sudan katika kipindi cha wiki moja, huku nchi ikikabiliana kudhibiti mlipuko mkubwa zaidi wa kipindupindi katika miaka mingi, shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limesema siku ya Alhamisi.
Shirika hilo la misaada ya matibabu linasema eneo kubwa la magharibi, ambalo limekumbwa na mapigano kwa zaidi ya miaka miwili kati ya jeshi na wapiganaji wa RSF, limeathirika zaidi na mlipuko hio wa mwaka mmoja sasa.
"Mbali za vita hivi, watu nchini Sudan sasa wanakabiliwa na mlipuko wa kipindupindu kibaya nchini humo," MSF ilisema katika taarifa.
Shirika hilo linasema vifo vilivyoripotiwa mwaka mzima hadi Agosti 11 kutokana na maambukizi ya kipindupindu, kati ya maambukizi 99,700.
"Katika eneo la Darfur pekee, maafisa wa MSF waliwatibu watu zaidi ya 2,300 na wengine 40 deaths walifariki katika wiki moja iliyopita," MSF iliongeza.
Maji machafu
Tangu jeshi kuchukuwa udhibiti wa mji mkuu Khartoum mwezi Machi, mapigano sasa yamehamia Darfur, ambapo wapiganaji wamekuwa wakijaribu kuchukuwa udhibiti wa mji wa El-Fasher.
Eneo hilo ndiyo mji wa mwisho mkubwa eneo la magharibi ambao bado uko chini ya udhibiti wa jeshi, na Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamezungumzia kuhusu hali mbaya kwa raia ambao bado wamekwama ndani ya sehemu hiyo.
"Katika kambi za wakimbizi wa ndani, familia zinalazimika kunywa maji kutoka vyanzi vichafu, na wengi wanapata kipindupindu," amesema Sylvain Penicaud, Mratibu wa mradi wa MSF katika eneo la Tawila.