AFRIKA
2 dk kusoma
Takriban waombolezaji 21 wafariki katika ajali ya basi nchini Kenya
Tukio la Ijumaa lilitokea katika Kaunti ya Kisumu baada ya basi - inaaminiwa kuwa lilikuwa linarudi kutoka kwenye mazishi mapema siku hiyo - kuanguka, kulingana na vyombo vya habari vya ndani
Takriban waombolezaji 21 wafariki katika ajali ya basi nchini Kenya
Faili: Polisi walisema dereva wa gari alipoteza udhibiti. / Reuters
tokea masaa 13

Basi lililokuwa limebeba waombolezaji kutoka kwenye mazishi lilipata ajali magharibi mwa Kenya siku ya Ijumaa, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 21, afisa mmoja alisema. Hii ni siku moja tu baada ya ajali za ndege na treni zilizoua watu 14.

Ajali hii ya hivi karibuni inafuatia ajali ya ndege karibu na mji mkuu Nairobi siku ya Alhamisi, ambapo ndege ya huduma ya matibabu ilianguka katika eneo la makazi na kusababisha vifo vya watu sita.

Siku hiyo hiyo, vyombo vya habari vya ndani viliripoti kuwa kulikuwa na mgongano kati ya treni na basi uliosababisha vifo vya watu wanane.

Ajali ya Ijumaa ilitokea majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za Kenya (1400 GMT) katika Kaunti ya Kisumu baada ya basi - linaloaminika kuwa lilikuwa likirejea kutoka kwenye mazishi mapema siku hiyo, kulingana na vyombo vya habari vya ndani - kupata ajali, Kamanda wa Trafiki wa Kanda ya Kisumu, Peter Maina, alisema.

‘Kupoteza usukani’

"Gari lilipoteza udhibiti, likapinduka na kuingia upande mwingine wa barabara," aliwaambia waandishi wa habari katika eneo la tukio.

"Tumepoteza watu 21, na kati ya hao 21 waliopoteza maisha ni wanawake 10, msichana wa miaka 10, na wanaume 10," alisema.

Watu watano walijeruhiwa vibaya katika tukio hilo, alisema, miongoni mwao ni mtoto wa miezi nane ambaye kwa sasa anapata matibabu katika hospitali ya karibu.

Chanzo cha ajali hiyo hakikuwa wazi, Maina alisema, akiongeza kuwa uchunguzi unaendelea.

Vyombo vya habari vya ndani viliripoti kuwa tukio hilo lilitokea katika sehemu ya barabara inayojulikana kwa ajali za mara kwa mara.

CHANZO:TRT Afrika
Kionjo cha TRT Global. Tupe mrejesho wako.
Contact us